KINACHOWAPONZA WANAWAKE NI BAADA YA WANAUME KUJUA HITAJI LAO KUU NI HARUSI BADALA YA NDOA
Machoni kwa watu kila Mwanamke anatamani kuwa na HARUSI ili aweke historia kwamba aliwahi kusanya watu wakashiriki nae kwenye FURAHA yake, kuliko wanawake wachache wanaohitaji NDOA ili wakawe WAKE ZA WATU
Ni fahari kubwa kwa wanawake wa leo KUVAA SHERA kwa sababu itamfanya apate tukio ambalo litampa PICHA ZA KUPOST Instagram, Facebook, Twitter hasa hasa WATSAPP
Ni raha kweli watu wakifurahi pamoja nawe katika azimio lako hilo, Tatizo langu kubwa JE MWANAUME UNAYE SHIRIKI NAE HARUSI ATAKUBALI KUKOMEA KWENYE HITAJI LAKO
Maana ili upate HARUSI lazima Uwe na mshirika ambaye ni MWANAUME hofu yangu ni namna gani itakuwa pale Mwanaume atagundua shauku yako ilikuwa HARUSI maana kama ni kazi unayo, unaweza kujihudumia na Mengine mengi unao uwezo wa kujitimizia ila lililokuwa gumu NI MWANAUME YUPI ATABAMBA SIKU YAKO YA HARUSI
Wanaume wengi wanaweza kushiriki HARUSI ila sio rahisi kumpata Mwanaume ambaye baada ya HARUSI atabakia kuwa BWANA HARUSI
Utii pekee wa Mwanamke ndiyo humfanya Mwanaume kumhurumia Mwanamke, japo kwa Dunia tuliyopo UMILIKI WA FEDHA umeharibu UTII kwa asilimia 78 ya wanawake wanawadharau sana wanaume, Japo Wanawake wasokuwa na kipato kikubwa kwamba Mwanaume ndiye mwenye nguvu ki uchumi hao wanaweza kutii, Tatizo lilianzia wapi?
MWANAUME KUKUBARI KULA CHAKULA AMBACHO HAJUI KIMEPATIKANA WAPI NDILO TATIZO LILIPOANZIA
Maana yake ni kwamba “MWANAMKE WA SASA ANAMPA KIPAUMBELE MWANAUME ALIYE CHINI YAKE KI MAPATO” ili aweze kumtuma, kumgombeza, kumkaripia na wengine kumtukana mwanaume haijalishi amezaa nae
Ndo maana kwa sasa NDOA ni kwa WASICHANA kuolewa na WAZEE kwa sababu hakuna mtu mzima anaweza kukubari atawaliwe na Mwanamke anayemzidi umri kwani hata MAANDIKO YANAKATAA MWANAMKE KUMTAWALA MWANAUME
Mwanamke Acha kufikiria HARUSI itakujenga kusubiri NDOA ambayo itatajwa na Mwanaume ambaye atakuwa MUME WAKO japo najua shida yenu ni MABEST kushare na shemela wao HANDSOME BOY
Sio kila Mwanaume atakuwa MUME wengi wapo kuleta ukombozi ki fikra tu, kama hutajua KUSOMA Basi kaa utafakari kwa KUANGALIA