IJUE THAMANI YA X ILA USIMPE NAFASI UKAKOSA MTU WA KUMFANANISHA KWENYE MAKOSA UWAPO KWENYE UHUSIANO MPYA
Mahusiano ama ndoa ili iwe na ukombozi lazima Kuwe na X aliyeharibu mtazamo hata ukaamua kuwa na mtu Mwingine, Mapenzi yanahitaji mwalimu ambae atakufundisha maana ya UPENDO WA KWELI na ule UPENDO WA SABABU
Ili kuijua kweli ya UPENDO mtu lazima uanze na mtu ambaye sio mkweli ili akufundishe kutofautisha, Maana kiumeni ni nadra Mwanamke kukutana na mkweli, Ndo maana waliobahatika kuolewa na walowabikiri hawaijui chungu ya MAPENZI ila pia hawaijui RADHA YA MAPENZI
Mapenzi hayana Mwalimu ila Muda wote ni kujifunza namna ya kukabiliana na MAUMIVU huku ukikomaa na kuelewa maana ya kubalance MAHUSIANO AMA NDOA
Usikubari X aendeshe hisia zako tena, Ukiweza kupambana na X ni rahisi kumjenga uliye nae ili awe Kwenye viwango upendavyo, X siku zote ni waharibifu wa juhudi uliyochukua Yaani hawatofautiani na shetani, kwamba kila unapokemea pepo TAMAA YA MALI inakujia
Epuka kitu kinaitwa X ili uweze kujenga HIMAYA YAKO VYEMA
Mahusiano ama ndoa ikiishakuwa IMEBUMA wala haina spare, kamwe hakuna MAREKEBISHO YA UPENDO ila tu ni Mtu mwenyewe kuamua kukubari MAUMIVU ama KUACHANA NA MAUMIVU kinyume chake wewe ni mhanga wa MAPENZI.