IJUE TOFAUTI YA MAPENZI NA UPENDO

💯
Kwanza kabisa nianze kwa kusema jambo moja kuu;-
👉🏼 HUWEZI KUTOFAUTISHA UPENDO NA MAPENZI LAKINI TOFAUTISHA MAPENZI NA UPENDO📍
Mtu unapokuwa na shauku ya MAPENZI ni eneo linalotokana na tamaa ya mwili pamoja na hisia juu ya hitaji husika la NGONO💉
Na mtu aliyewaka tamaa ya NGONO hawezi kuzalisha UPENDO WA MOYONI ila anaweza kuzalisha UPENDO WA MWILI maana hata mapenzi bila kuyapenda nadhani huwezi kuwa na sababu ya kuwa na mtu😂
Lakini pia UPENDO ni zao la haja ya moyo na mara zote huwa naamini MWENYE UPENDO NI RAHISI KUTOA PENZI LENYE MAANA ZAIDI kwa sababu kilichozaliwa ndani yake ni UTASHI na kama mwenye UPENDO akiwa katika kweli yake swala linaitwa MAPENZI hutokana na utimilifu wa adhima yake ikiwemo kusubiri.
Kuna watu wanayataka MAPENZI kwa kisingizio cha UPENDO ila wenye UPENDO WA DHATI hawaangaliii katika MAPENZI maana ni rahisi MAPENZI kutengenezwa katika UPENDO💯
Ila ni ngumu sana MAPENZI KUTENGENEZA UPENDO NJE YA NGONO na hapo ndipo anguko la maana halisi ya UPENDO HUANZIAA.
Mwili unapowaka tamaa ya NGONO akili huyumbishwa kiasi kwamba Mtu unaweza kuamini UNAMPENDA Mtu fulani na kumbe akikupatia hitaji lako AUTOMATICALLY ile hali ulikuwa unaisikia inatoweka😂😂
Na JOTO LA UPENDO 💘 likipanda juu ya mtu fulani shauku yako ni kutaka kujua kama UPO KWENYE MOYO WAKE PIA na mara nyingi mwenye UPENDO WA DHATI 💘 akiisha pewa nafasi huongelea hatma ya safari ya MAISHA wala sio NGONO maana anaamini mwisho wa siku ni UMILIKI WA KUDUMU📍
Ndo maana hata Maandiko Matakatifu yanasema :-
👉 USIYACHOCHEE MAPENZI BALI YAACHE YAJITENGENEZE MENYEWE.
Image may contain: one or more people, ocean, sky, outdoor and nature

DOWNLOAD APP YETU GOOGLE PLAY BONYEZA HAPA

DOWNLOAD APP YETU GOOGLE PLAY BONYEZA HAPA