USIRUHUSU WATU WANAOKUZUNGUKA KATIKA MAISHA YAKO KUKUFANYIA MAAMUZI YAKO!






Dada mmoja aliniambia, ninatamani sana kufanya biashara lakini kila mtu ninayemuomba ushauri ananiambia biashara ni ngumu na kwa namna nilivyo sitaweza. Watu wananiambia kua siwezi kuhangaika kutafuta mzigo, Baba yangu ananiambia ni bora kutafuta kazi ya kuajiriwa kwani mimi ni mpole sana hivyo ninaweza kutapeliwa na kuishia kulilia. Mpenzi wangu ananiambia atanipa kila kitu hivyo sina haja ya kujisumbua kwani biashara ni ngumu sitaweza.

Lakini kaka mimi nina hamu sana ya kufanya biashara ila najiona kama siwezi kwani hata Mama yangu mzazi ananiambia kua siwezi kufanya biashara. Nilimuangalia na kushangaa, kwanza hakuna mtu ambaye kazaliwa ili kufanya biashara na suala la mafanikio halijalishi kama unalia au hulii, kama umwembamba au mnene, kama u mwanamke au mwanaume ananiambia anataka kuchukua mkopo ili ampe mchumba wake na wafungue biashara kwa pamoja mchumba wake aisimamie kwani yeye hawezi kusimamia.

Nilimuambia asubiri nitampa jibu, baada ya wiki moja nilimtafuta na kumuambia, unaonekana una umwa, kwa namna unavyoonekana utakua na Malaria, lakini inawezekana una UTI na aleji, aslinishangaa sana na kunaimbia yeye yuko sawa na wala hana tatizo lolote. Nilizidi kumkazania kua anaumwa na anahitaji kwenda kupima alikataa na mimi nikamkazania akapime kwani ni mgonjwa. Nilimuambia kwa kumuangalia tu najua anaumwa asipokua makini Malaria itapanda kichwani na anaweza kufa.
iddimakengo #part2 #anziapostiliyopita

Alipata hofu na kwenda kupima, alipima kila kitu na hakukutwa na ugonjwa wowote, alikuja na kuniambia hana akanionyesha na majibu. Nilimuambia nilijua kabisa hana, akaniuliza sasa kwanini nilikua namuambia ni mgonjwa nikamuambia “Mtu anaweza kukuambia chochote lakini haimaanishi kinaukweli. Watu wanaokuzunguka wanakuona mdhaifu, wanakuona kama huwezi biashara, wanakuona huwezi kudilia na mikiki mikiki ya maisha lakini hiyo haimaanishi kua ni kweli, ukweli unao wewe na kama utayaruhusu maisha yako yaamuliwe na maneno ya watu basi hutakuja kufanikiwa.”

Nikamuambia katika maisha kuna watu wa aina mbili, aina ya kwanza ya watu ni wale ambao wakiambiwa kitu flani huthibitisha kwanza kabla ya kuamini na wale ambao wakiambiwa kitu huamini tu. Nilimuambia nilipokuambia unaumwa hukuamini, ulienda kupima kwanza lakini umeambiwa huwezi kufanya biashara unawaamini hao watu hata kabla ya kujaribu kufanya biashara. Huwezi kushindwa kitu kwakua flani kasema huwezi unashindwa kwakua wewe umesema huwezi hivyo nenda kawaonyeshe kua unaweza!

Katika maisha uamuzi ni wako na si wa watu wengine, wewe ndiyo uanjijua zaidi kuliko watu wengine. Kwakua watu wanasema kitu flani haimaanishi kua ni kweli, haimaanishi kua kitatokea, na wala haimaanishi kua unatakiwa kuwasikiliza. Kuna watu wengi sana wanashindwa kutimiza ndoto zao kwakua tu waliambiwa kua hawawezi. Bahati mbaya nikua wakiambiwa hivyo wanaamini bila kukumbuka kua watu wengi wanaokuambia kua huwezi ni wale ambao wao wenyewe walijaribu na wakashindwa! Acha kuwasikiliza watu wanaokukatisha tamaa, tafuta sauti ndani ya moyo wako inayokuambia twende unaweza.

DOWNLOAD APP YETU GOOGLE PLAY BONYEZA HAPA

DOWNLOAD APP YETU GOOGLE PLAY BONYEZA HAPA