πŸ‘‰1.KILA UNAEMUOA AU KUOLEWA NAYE ANA UDHAIFU WAKE.*

 *


Mungu
pekee ndio hana udhaifu,
Kila ua waridi lina chimbuko lake.
*πŸ‘‰2.KILA UNAEMUOA AU KUOLEWA NAYE ANA HISTORIA YAKE MBAYA.*
Hakuna mtu ambaye ni malaika,
epuka kuchunguza mambo ya mtu ya nyuma samehe na usahau.
*πŸ‘‰3.KILA NDOA INA CHANGAMOTO ZAKE*
Ndoa sio kitanda cha maua waridi yanayomeremeta kila muda,
kila ndoa yenye mafanikio imepitia misukosuko mingi.
*πŸ‘‰4.KILA NDOA INA HATUA ZAKE KATIKA MAFANIKIO*
Hatuwezi kuwa sawa,
kuna watakaokuwa mbele kidogo na watakaokuwa nyuma kidogo. Kupunguza stress, kuwa mtulivu, fanya kazi kwa bidii na kwa muda muafaka ndoto za ndoa yako zitatimia.
*πŸ‘‰5.KUOA AU KUOLEWA NI KUTANGAZA VITA*
Ukishaoa au kuolewa ni kuingia katika uwanja wa mapambano,
Kuwa tayari kupambana kuulinda ukanda wa ndoa yako.
*πŸ‘‰6.HAKUNA NDOA ILIYOKAMILIKA.*
Hakuna ndoa ambayo imetimilika,
Ndoa ni kazi ngumu,
jitolee mwenyewe na ufanye kazi ya kuijenga ndoa yako iwe kamilifu.
*πŸ‘‰7.MUNGU HAWEZI KUKUPA MTU KAMILI UNAYEMTAKA.*
Mungu atakupa mtu ili wewe umtengeneze jinsi wewe unavyohitaji yeye awe.
*πŸ‘‰8.KUOA /KUOLEWA NI KUJIINGIZA KATIKA HATARI.*
Huwezi jua nini kitatokea baada ya ndoa,
hali inaweza badilika,
hivyo achia nafasi ya marekebisho.
*πŸ‘‰9.NDOA SIYO MKATABA WA MUDA BALI NI MKATABA WA KUDUMU.*
Ndoa inahitaji ahadi ya kudumu,
mapenzi ni gundi ambayo huwafanya wanandoa kuwa pamoja daima..
Talaka huanza katika mawazo.
*πŸ‘‰10.KILA NDOA HUHITAJI KUJITOA.*
Hakuna mapenzi rahisi katika ndoa,
huwezi kupenda au kupendwa bila kujitoa nafsi yako kwa dhati...
Share
May be an image of flower

DOWNLOAD APP YETU GOOGLE PLAY BONYEZA HAPA

DOWNLOAD APP YETU GOOGLE PLAY BONYEZA HAPA