Kuna kosa la kiufundi ambalo Wanandoa wengi wanalifanya,
na mwisho wa siku linawapeleka kwenye usaliti wa *NDOA* zao au kujikuta wamezini. Kosa lenyewe ni kuwa *KARIBU* sana na mtu ambaye si *MKE*
wako au *MUME*
wako!.
Wanandoa wengi wamekuwa wakianzisha ukaribu au urafiki wa karibu sana na mtu ambaye si *MKE*
wake au *MUME*
wake.
Na mara nyingi wanakuwa karibu kiasi ambacho wanajikuta wakielezana mpaka matatizo au changamoto zinazowakabili na wenza wao. Ukaribu huu huwapelekea kujiona salama, wakiwa na furaha na amani Kuliko wakiwa na wenza wao na mwisho wa siku wanajikuta wameangukia kwenye *UZINZI.*
*EWE MWANAMDOA* ni hatari sana kuwa na urafiki wa karibu na mtu ambaye si *MKE*
wako au *MUME"* wako.
Tena unakuta mnakutana sehemu mkiwa wawili Mkielezana changamoto zenu za *NDOA*
huku mkifarijiana au mnasema mnaenda kujiliwaza! Tambua lazima mtaangukia kwenye *UZINZI*
tu.
Usalama ni upi sasa?
Sikiliza Usalama ni *WEWE* kujenga urafiki na Mwenza wako,
tumia akili *ZAKO ZOTE,* Maarifa yako yote *KUHAKIKISHA*
Mwenza wako anakuwa rafiki yako. Hakikisha Mwenza wako ndiyo anakuwa mtu wa Kwanza kukutia moyo, kukushauri,
na kukuliwaza au kuwa msiri wako.