JINSI YA KUMUHESHIMU MUMEO








1. Wasiliana nae kwa upendo na adabu. Usiongee nae kwa hasira, dharau na kejeli.


2. Mwache ajue kwamba yeye ni wa muhimu kwako. Kila siku muonyeshe hilo.


3. Elewa hisia zake, hata kama mtakua mna mabishano, Basi bishana kwa upole na sio kumpandishia sauti.


4. Onyesha kuwajali rafiki zake kwa kumpa muda wa kukaa nao ila ni kama marafiki wa kuaminiwa.


5. Jaribu kupotezea mambo madogo madogo. Tunatofautiana katika tabia na mwenendo. Mambo mengine ni ya kuchukuliana na si kuibua ugomvi.


6. Mwambie kuwa unampenda na unamhitaji.


7. Onyesha kujali yale mambo anayoyapenda, kama ni mpenda mpira mnunulie hata jezi ya timu aipendayo. Wanunulie watoto pia jezi kumsupport baba yao.


8. Linda utu wake popote pale. Usimuongelee vibaya aitha kwa ndugu au mashoga zako. Usiruhusu hata rafiki zako wamseme vibaya.


9. Hata akikukosea, tambua na yeye ni binadamu sio malaika.


10. Tengeneza mazingira ya furaha na tabasamu ktk mahusino yenu. Tafuta njia ya kucheka na kufurahi pamoja.


11. Usijaribu kufanya mabadiliko ya ghafla, mueleze ili apate muda wa kuendana na mabadiliko hayo.


12. Mkiwa mmeenda sehemu kujipumzisha na ku enjoy, usilete matatizo ya nyumbani na kuanza kuyaongelea hapo. Enjoy nae pasina mikwaruzano.


13. Jikite kwa yale mazuri anayofanya kwa ajili ya familia, msamehe kwa yale mabaya anayofanya. Sheherekea yale mazuri na muombee kwa yale mabaya.


14. Onyesha kujali kile anachohisi ni muhimu ktk maisha.


15. Mpe muda wako, usitumie muda huo kichezea simu yako.


16. Usiruhusu ndugu zako wamkosee heshima. Mlinde kwa yeyote yule atakemshushia heshima mfalme wako.


17. Msifie na mtie moyo kwa kila jambo zuri analofanya.


18. Kuwa mbunifu pale unapoonesha mapenzi yako kwake katika vitendo na maneno.


19. Ongea nae kuhusiana na uchumba wenye tija, malengo ya kifamilia na jinsi ya kuyafikia, uchumi na biashara.


20. Usimbane na kumchunguza sana kana kwamba ni mhalifu ambae atakukimbia. Mpe muda usimbane.


21. Kubali makosa yako. Usiwe mwoga kuwa mnyenyekevu. Usijivunie uzuri wako. Wapo wazuri wengi tu. Ila amekuchagua wewe.


22. Mtumie text wakati yupo kazini, mwambie ni jinsi gani unampenda.


23. M-suprise na zawadi, sio vitu vikubwa..boxer, saa, tshirt etc..atakuona unamjali!


24. Mwambie ni jinsi gani unavyothamini jitihada zake katika kuandaa mazingira yenu mazuri ya baadae.


25. Mpe chakula kitamu akipendacho, nazungumzia vyote cha mezani na cha usiku. Usitumie sex kama silaha ya kumkomoa. Definetly ataenda kutafuta nje tu!


26. Maongezi yako yawe mafupi pale anapokuwa amechoka, ana hasira au ana njaa. Jifunze kutokua muongeaji sana.


27. Wasilisha maombi yako au mahitaji yako ktk njia ambayo ipo romantic kwa kumbembeleza..kumfanyia 'massage' na kumpapasa usoni.


28. Ni hulka ya wanaume na ndivyo walivyoumbwa kutokua wasikivu, ni vema ukalitambua hilo na ukalichukulia kama changamoto kuliko kulaumu.


Ni matumaini yangu haya yote yanawezekana. Jaribu kuyafanya ili udumishe mahusiano yako.


MWISHO

DOWNLOAD APP YETU GOOGLE PLAY BONYEZA HAPA

DOWNLOAD APP YETU GOOGLE PLAY BONYEZA HAPA