JE MAHUSIANO YAKO HIVI??
Unapokuwa katika mahusiano ambayo unategemea yaishie katika Ndoa, huwa kuna Taa nyekundu ambazo huwaka kuashiria hali ya hatari kuhusiana na mtu uliyenae kwenye mahusiano.
.
Sikiliza kwa makini. Kama Mpenzi wako sio aina ya mtu ambaye unatamani uwe nae kwenye Ndoa, Basi Ndoa haiwezi kumbadilisha.
.
Kama kila siku ninyi ni ugomvi tu Jumatatu mpaka Jumatatu, Ndoa haiwezi kuwa-guarantee kuwa na masikilizano baada ya kuingia humo.
.
Watu wawili hawawezi kutembea pamoja wakaifurahia safari kama hakuna Mapatano. Upatano ni muhimu sana katika urafiki, mahusiano na Ndoa.
.
Kama mpenzi wako ni mtu wa kukuumiza kila iitwapo leo, mtu wa kukushusha thamani na kutokukuheshimu usije kufikiri labda Mkiingia kwenye Ndoa atabadilika.
.
Ndoa sio gereji ya kurekebisha tabia. Ndoa ni maisha ya uhalisia. Usiseme unampa muda wa kubadilika, ni vigumu kubadili tabia ya mtu mzima. MUNGU pekee ndiye anayeweza kumbadilisha mtu.
.
Mapenzi yasikupige upofu ukashindwa kuona Taa nyekundu. Wewe ni mtu mwenye thamani yako, sio mtu wa majaribio!