Ijue tofauti ya USALITI wa Mwanamke na Mwanaume;-
USALITI WA MWANAMKE
Ni shauku ya kutafuta AMANI baada ya kuona mahusiano au ndoa yake haikuwa kama alivyotarajia, na mara nyingi Mwanamke hukomea hapo asiweze kuchukuwa hatua nyingine, labda kama Mwenza aliye nae haonyeshi mabadiliko yoyote
USALITI WA MWANAUME
Mara nyingi ni TAMAA japo kuna wanaume wengine ni UPENDO kwa mtu wa pili, Ndo maana wanaume walio wengi akisaliti anaweza kujikuta AMEMZALISHA MWANAMKE HUYO na wengine hata kumfanya mke mdogo
Yote ni usaliti, na lazima Maumivu yachukue nafasi yake, mwisho wa usaliti ni KUACHANA kwani hakuna aliyesalitiwa akabakia Kwenye msamaha na kuachilia zaidi ile hali ya MALIPIZI hutawala Muda wote, Kama Mtu anajua THAMANI YAKO KWA VYOVYOTE VILE ANAWAJIBIKA KUKUBEBEA MADHAIFU YAKO
Vinginevyo wewe sio wa moyo wake ndo maana anajaribu kutafuta Mwingine huko nje, na wakati akiendelea kutafuta lazima AKUSALITI na hiyo ndiyo Maana kwamba wewe sio wake