MCHUMBA WANBU ANATAKA KUNIACHA MWEZI MMOJA KABLA YA HARUSI?
iddimakengo
Ndoa yangu ni mwezi wa pili kaka, niko kwenye mahusiano huu ni mwaka wa nne, sijawahi kumsaliti mpenzi wangu wala kuhisi kufanya hivyo. Ila Kaka kuna tatizo moja na sijui nafanya nini, kuna Kaka mmoja kwenye mitandao tumezoeana, sijawahi kuonana naye wala hata kuongea naye ila huwa napenda kucomennt kwenye picha zake na kila kitu anachopost.
Yeye pia hufanya hivyo kwenye ukurasa wangu, kwasababu hiyo tumejikuta tunakua marafiki na mara nyingi tunakua tukichart mambo ya kawaida. Anajua nina mchumba wangu na tumezoeana kiasi kwamba mambo yangu na mchumba wangu namuambia, mwezi uliopita nilimuambia kuwa ninaolewa.
Alinipongeza na kuniambia kuwa atanipa mchango kwenye harusi yangu, basi kwa mara ya kwanza akaniomba namba ya simu nikampa akanitumia laki tatu. Baada ya kunitumia tukawa tunachart tu tunajuliana hali na vitu kama hivyo. Mimi niko Dar na yeye anaishi Arusha, wili iliyopita alinaimbia kuwa anakuja Dar na akipata muda basi atataka kuja kuniona kabla ya ndoa basi nilimuaomba sawa kama rafiki.
Kweli alikuja na weekend hii aliniambia sehemu ambapo kashukia basi mimi nikaenda kuonana naye. Alishukia hoteli kubwa tu, nilimuaga mchumba wangu kuwa naenda kuonana na rafiki yangu, kwakua najua wanaume walivyo na wivu sikumuambia kuwa ni rafiki wa kiume. Nilienda kweli aliposhukia, sikuingia chumbani, nilienda kukutana naye sehemu ya wazi tukaongea mpaka jioni.
Wakati nipo kule kwa bahati mbaya simu yangu ilizima chaji, nilikaa mpaka kwenye saa mbili hivi ndiyo yule Kaka kwakua alikua na gari alinirudisha nyumbani. Kumbe kipindi chote hicho simu yangu haina chaji mchumba wangu alikua akinitafuta kwenye simu, nilifika nyumbani yule Kaka alinishusha na kuondoka, wakati huohuo ananishusha mchumba wangu naye ndiyo alikua anaingia.