MWANAMKE NAKUITA HAPA USOME UPATE KUJUA NI MWANAUME YUPI ANAJUA THAMANI YAKO

Kwanza fahamu kwamba;-


Mwanaume ni jinsia ila kupata wa kukupenda anatakiwa awe Mwanaume ajuaye NAFASI YAKO KWAKE Maana katika kutafuta THAMANI yako kwa Mwanaume lazima uwe na mtu ambaye kila akijaribu kukuwekea vikwazo anajihisi ni mkosaji.
Mwanaume kama bin adam anaweza kujiona Yupo sahihi katika kosa ambalo amekufanyia ukajisikia vibaya na wakati Mwingine ukaona siku yako kuwa mbaya, lakini kwa ufahamu wake akajua unyonge wako umesababishwa na yeye na akainuka kukusemesha ama kukutumia ujumbe na kusema neno la kurejesha FURAHA NA AMANI yako huyo ni wa kumshika, Mwanaume kwa uhalisia wake ni MMILIKI WA MFUMO DUME kwamba yeye hata kama ni mkosaji Basi analazimisha Mwanamke awe chini tu

Lakini ukiona Mwanaume anajisahihisha mwenyewe ama kosa lako halikupashwa kuadhibiwa kama ulivyo adhibiwa, ama namna ya kukuelekeza kwa makosa yako hakufikisha ujumbe kwa hekima ila alitumia hasira, Mwanamke fahamu nature ya mwanaume sio watu wa kubalance hasira zao, ila ukiona Mwanaume anarudi kwako baada ya kukuumiza ama kukuonea ujue tu;-


Maana yake huyo anao uwezo wa kutofautisha kati ya HASIRA NA UPENDO ndo maana amejua kosa lake ama amejua THAMANI yako.