UNALIJUA JUKUMU LAKO KWENYE MAHUSIANO/NDOA YAKO


🤷‍♂️
Kumekuwa na mahusiano na ndoa nyingi watu hawajui jukumu lao hasa ni lipi kwa wenza wao, Muda mwingine uvunjifu wa PENZI husababishwa na mtu kutojua jukumu lake, na hilo ndilo linaacha nyufa Kwenye MAPENZI 🤔
Uko na mtu lakini kama alijua jukumu lake ni mwanzoni mnaanza, baadaye wala asishughurike na kile alijua ndicho kinacho imarisha UPENDO wako kwake, Kwenye MAPENZI kama hujui jukumu lako kwa mwenza wako niamini kama hujasababisha USALITI basi utavunja kabisa UHUSIANO AMA NDOA yako, Kwa sababu kinachovutia MTU ni kile aliamini wewe ndiye uwezaye kumpatia, na kama unajiona wewe ni zaidi ya wengine basi endelea kujiona CAKE 🎂 ili wakati ukifika umtafute ELISTA akupe ushauri ikiwa wewe mwenyewe ulishindwa kusoma alama za nyakati🌈
Kama huwezi kujua jukumu lako Kwenye MAHUSIANO AMA NDOA basi wewe ni mtu wa ajabu Sana, Na inawezekana ukaendelea kulalamika huna bahati ya kupendwa na kumbe wewe ni MENEJA WA MAPENZI Yaani ukipendwa na kupewa nafasi kubwa una RELAX😂😂
Mwanangu Kwenye MAPENZI ni kutwa na Usiku unakukuruka, Yaani ni kama sisimizi kila ilipo SUKARI nawe upoooo, Vinginevyo hutaona Mtu sahihi, Maana wewe hujui JUKUMU lako Kwenye MAHUSIANO AMA NDOA YAKO💯
May be an image of 1 person, child and outdoors

DOWNLOAD APP YETU GOOGLE PLAY BONYEZA HAPA

DOWNLOAD APP YETU GOOGLE PLAY BONYEZA HAPA