MWANAUME ACHA KULAUMU, HEBU MFANYIE MKEO AU MPENZIO HAYA UONE TOFAUTI

1. Mpe muda wako. Usimfanye aombe muda wako. Tengeneza muda kwa ajili yake. Tengeneza wakati ambao mtakuwa mkifurahi na kupiga story pamoja. Usiwe bize Jumatatu mpaka Jumapili. Wanawake hupenda sana kusikilizwa na waume zao.

2. Msifie pale anavyofanya jitihada ya kuwa na muonekano mzuri. Pale anaposuka mitindo mipya ya nywele, anavyovaa nguo nzuri na hata anapokupikia chakula kitamu. Mwanamke husikiliza mno maoni ya mwanaume ampendae. Mu-appreciate mke wako, nae atafanya kila kitu kwa ajili yako.

3. Wanaume ni wazito kusema "samahani". Yani kuna wanaume anajua kabisa kakosea lakini anaona akimwambia mkewe au mpenzi wake samahani ni kama amedhalilika au amedharaulika. Sikiliza, iko hivi hili neno samahani wala halikupunguzii uanaume wako. Kuomba msamaha sio UDHAIFU, mashujaa na watu wenye nguvu na hekima ndio wanajua siri na nguvu iliyopo ndani ya neno samahani. Pale unapomkosea muombe Msamaha. Hii itaonesha ni kwa kiasi gani unathamini moyo wake. 

4. Mnunulie zawadi, hata kama ni kitu kidogo na cha bei ndogo. Mwanamke anayekupenda hua hajali gharama, anajali alama na jitihada zako kwamba atleast unamkumbuka ktk fikra zako kiasi cha kumpa zawadi fulani.

5. Muombe ushauri katika perspective mbalimbali. Hata kama unajua huwezi kutumia ushauri wako. Wewe muombe tu hivyo hvyo. Hii itamuweka katika nafasi ya kujiona unamthamini katika mipango yako.

6. Mbusu bila sababu, mguse na kumshika bila sababu ya msingi. Yeye ni mali yako unayo haki hiyo. Mfanye ajisikie kwamba unamhitaji leo jana na kesho.

7. Mtreat vizuri siku zote, sio pale tu unapotaka tendo la ndoa. Kwa kufanya hivyo utamfanya hata siku ya ku-make love afurahie tendo to the maximum. Tendo la ndoa kwa wanawake ni hisia, ukiumiza hisia zake, hata tendo la ndoa litamuumiza. Jali moyo wakez nae atakuonyesha maajabu katika tendo.

8. Muangalie usoni unapoongea muelekeze pale anapokosea, usimkosee heshima na kumuonesha wazi kabisa kwamba ana-share na wengine huko nje. Moyo wake utakufa ganzi.

9. Msaidie kazi za nyumbani na malezi ya mtoto/watoto. Ni mwanamke uliyempenda, ukamchagua na kumuoa. Hivyo ni msaidizi wako sio kijakazi, sio mtumwa wako. Mwanamke ni msaidizi wako.

10. Mpe moyo pale anapojihisi kukata tamaa, mtie moyo, mkumbatie pale anapojihisi yupo down. Kuwa upande wake pale anapoonewa wazi kabisa na familia yako. Faraja kubwa ya mke ipo kwa mumewe. 

Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; Bali mwanamke amchaye BWANA, ndiye atakayesifiwa.....Mithali 31:30.

Remmy Cameroon  
Sauti ya wasio na sauti

DOWNLOAD APP YETU GOOGLE PLAY BONYEZA HAPA

DOWNLOAD APP YETU GOOGLE PLAY BONYEZA HAPA