ZAO LA UPENDO ❤️ HUSITAWISHWA ZAIDI NA NINI UNAFANYA KWA ALIYEKUPENDA💯


Moyo ni shuhuda wa nini mtu anafanya kwako ikiwa wewe umeamua kumchagua awe wako kwa UPENDO WA DHATI ❤️
Huwezi kupewa UPENDO kama wewe hujaonyesha sauti ya matendo yatokanayo na UPENDO kwani tabia ya NAFSI ni uhakiki wa nini unafanya kulingana na vile NIMEKUPENDA.
Muda Mwingine mtu akipendwa huona kama sheria😂
Ni kweli MUNGU anaagiza UPENDO kwa wengine ila ni kwa ajili ya UBIN ADAM📍
Unapozungumzia UPENDO WA MAHUSIANO NA NDOA huo unahitaji MAPOKEO YA MAPENDO unipende nami nikupende bila kujiangalia wewe ni nani ila ni kwa sababu hiyo hiyoooooo kwamba;-
👉🏼 TUNAUNGANISHWA NA MAPENZI.
Huwezi kutaka UPENDO halafu mtu akajua unamtumia kwa maslahi yako akabakia na UPENDO HALISI⛔️
Kila mara nasema;-
👉🏼 MOYO NI MWOGA SANA KAMA HAUJAPATA HAKIKA YA UPENDO.
Tafuta kuaminiwa na NAFSI japo moyo ndiyo mjumbe wa UPENDO lakini IMANI YA UPENDO huzaliwa na NAFSI💯
Tafuta kuwa mwenye FURAHA NA AMANI kwa kulinda IMANI YA UPENDO kwa mwenza wako, Huwezi kuwa na Mtu halafu unataka yeye akupende ila wewe humpendi halafu ukadumu katika UPENDO WA MWINGINE⛔️
UPENDO una tabia ya kuambukizana matendo ya UPENDO ni rahisi kuwa katika PENDO IMARA kama hakuna unafiki📍
Mpende anayekupenda na kuijua THAMANI yako, Kama hujaona UPENDO wake na hujui kama ana thamani uwepo wako kwake PIGA CHINI HARAKA unapoteza muda🕺🏻
Muda Mwingine wanaotuhadaa ni wale wanaotafuta PANADOL baada ya HOMA ZA MAHUSIANO NA NDOA zao, hao ndio wengi kuliko wenye NAFASI PANA MIOYONI MWAO na ukimpata huyo mjenge katika hakika ya UPENDO ❤️
May be an image of one or more people, beach and ocean

DOWNLOAD APP YETU GOOGLE PLAY BONYEZA HAPA

DOWNLOAD APP YETU GOOGLE PLAY BONYEZA HAPA