🌹ADABU YA MUME KWA MKEWE.🌹

 


*💕 Usitangaze udhaifu wa mkeo kwa familia na marafiki, kila mmoja*
*anamtunzia mwenziwe hadhi yake.*
*💕 Usiwe na mtizamo mbaya wala kuzungumza naye kwa hisia kali*
*huwezi kujua atatafsiri vipi.!!*
*💕 Usimlinganishe mkeo na wanawake wengine, huwezi kujua hao wanawake*
*wengine wanapitia hali gani kimaisha, kila mwanamke anasifa zake.*
*💕 Usisahau kwamba ni mkeo umemuoa, yeye si kijakazi, muhudumie kama malikia na atauonyesha ulimwengu kwamba*
*Mumewe ni mfalme na utamtawala maishani.*
*💕 Mpe kipaumbele na ni wajibu wako binafsi kumfanyia jambo na sio watuwengine.*
*💕 Usimlaumu mbele za watu hata kama kakosea, mlinde, muhimize, mrekebishe faraghani, ukifanya hivyo kamwe hatokusahau.*
*💕 Usimnyime huduma za kitandani kwa kujifanya mgonjwa/kuchoka ama*
*kutokuwa na hamu, kumbuka wanaume wengine wanatafuta nafasi*
*hiyo.*
*💕 Usimlinganishe mkeo na mtalaka wako ama mkeo aliyefariki maana wewe ni mume wa pekee kwake.*
*💕 Usimkemee wala kumkosoa mbele*
*ya watoto, ni malezi mabaya kwa watoto maana wewe ni mwalimu wao, wanakutazama wewe japo unadhani ni watoto tu!!.*
*💕 Mtazame mkeo kama kavaa vizuri kabla hajatoka maana akipendeza yeye na wewe unaheshimika na*
*ukipendeza wewe yeye anaheshimika.*
*💕 Usikubali marafiki kuwa karibu na mkeo, weka mipaka maana hujui nia*
*zao.*
*💕 Usitoke kuoga na haraka haraka ukavaa nguo ukatoka pasi yeye kukukagua, mkeo kazungukwa na wanaume wanadhifu wanaojali*
*mazavi na utanashati.*
*💕 Wazazi, ukoo na marafiki sio waamuzi kwa mambo ya mkeo, usipoteze muda kutafuta uamuzi wa*
*mwisho kutoka kwao, ithibiti ndoa yako.*
*💕 Mapenzi yako yasiwe kwa sababu ya mazingira au kihali hata kama ulimuoa kwa misingi hiyo kwa sasa ni*
*mkeo mpende bila masharti, hali uweza kubadilika na ikiwa ndio msingi*
*basi ndoa itavunjika.*
*💕 Mkeo anahitaji umakinike kwake na umsikilize kama mtoto, usiwe mkali msikilize kwa makini na atakupenda.*
*💕 Usijilinganishe na mkeo, yeye ni mke kwa hivyo msaidie tu maanandoa ni kusaidia.*
*💕 Usimuhukumu mkeo, ni msaidizi wako na kiumbe dhaifu mchukulie kwa mtazamo huo na utapata utulivu wa akili.*
*💕 Mume mzembe hajali, haogi, jiweke nadhifu ukiwa na yeye nukia vizuri, harufu mbaya inamkirihisha ila*
*hawezi kukwambia.*
*💕 Usiwe na urafiki na waume walio na mtazamo mbaya kuhusu ndoa.*
*Watakuharibu mawazo.*
*💕 Mkeo ana thamani kubwa sana ndio maaana ukatoa vitu vya thamani*
*kumuoa, penzi lenu lifanye jipya, uzembe haufai.*
*💕 Kuzaa ni majaaliwa,* *mpende mkeo awe na watoto au asiwe nao,*
*usiwabague watoto kwa jinsia wafunze dini na watakuwa wacha*
*Mungu hadi maishani mwao.*
*💕 Hauwi mzee kwa mkeo katika kumburudisha, usiwe na ugomvi naye*
*mutakuwa katika kheri, usiwache kuwajali watoto wako na mkeo kwa*
*sababu ya wanawake wengine au sababu yoyote ile, wao ni wewe na*
*wewe ni wao.*
*💕 Mume anayedumu na ibada ana usalama, omba kila siku, muombee*
*mkeo na watoto.*
*💕TUKIYAFANYA HAYA TUTAKUWA* *NA NDOA BORA MNO!!💕*
May be an image of 1 person, standing and car

DOWNLOAD APP YETU GOOGLE PLAY BONYEZA HAPA

DOWNLOAD APP YETU GOOGLE PLAY BONYEZA HAPA