🌹ADABU YA MUME KWA MKEWE.🌹
*
Usitangaze udhaifu wa mkeo kwa familia na marafiki, kila mmoja*

*anamtunzia mwenziwe hadhi yake.*
*
Usiwe na mtizamo mbaya wala kuzungumza naye kwa hisia kali*

*huwezi kujua atatafsiri vipi.!!*
*
Usimlinganishe mkeo na wanawake wengine, huwezi kujua hao wanawake*

*wengine wanapitia hali gani kimaisha, kila mwanamke anasifa zake.*
*
Usisahau kwamba ni mkeo umemuoa, yeye si kijakazi, muhudumie kama malikia na atauonyesha ulimwengu kwamba*

*Mumewe ni mfalme na utamtawala maishani.*
*
Mpe kipaumbele na ni wajibu wako binafsi kumfanyia jambo na sio watuwengine.*

*
Usimlaumu mbele za watu hata kama kakosea, mlinde, muhimize, mrekebishe faraghani, ukifanya hivyo kamwe hatokusahau.*

*
Usimnyime huduma za kitandani kwa kujifanya mgonjwa/kuchoka ama*

*kutokuwa na hamu, kumbuka wanaume wengine wanatafuta nafasi*
*hiyo.*
*
Usimlinganishe mkeo na mtalaka wako ama mkeo aliyefariki maana wewe ni mume wa pekee kwake.*

*
Usimkemee wala kumkosoa mbele*

*ya watoto, ni malezi mabaya kwa watoto maana wewe ni mwalimu wao, wanakutazama wewe japo unadhani ni watoto tu!!.*
*
Mtazame mkeo kama kavaa vizuri kabla hajatoka maana akipendeza yeye na wewe unaheshimika na*

*ukipendeza wewe yeye anaheshimika.*
*
Usikubali marafiki kuwa karibu na mkeo, weka mipaka maana hujui nia*

*zao.*
*
Usitoke kuoga na haraka haraka ukavaa nguo ukatoka pasi yeye kukukagua, mkeo kazungukwa na wanaume wanadhifu wanaojali*

*mazavi na utanashati.*
*
Wazazi, ukoo na marafiki sio waamuzi kwa mambo ya mkeo, usipoteze muda kutafuta uamuzi wa*

*mwisho kutoka kwao, ithibiti ndoa yako.*
*
Mapenzi yako yasiwe kwa sababu ya mazingira au kihali hata kama ulimuoa kwa misingi hiyo kwa sasa ni*

*mkeo mpende bila masharti, hali uweza kubadilika na ikiwa ndio msingi*
*basi ndoa itavunjika.*
*
Mkeo anahitaji umakinike kwake na umsikilize kama mtoto, usiwe mkali msikilize kwa makini na atakupenda.*

*
Usijilinganishe na mkeo, yeye ni mke kwa hivyo msaidie tu maanandoa ni kusaidia.*

*
Usimuhukumu mkeo, ni msaidizi wako na kiumbe dhaifu mchukulie kwa mtazamo huo na utapata utulivu wa akili.*

*
Mume mzembe hajali, haogi, jiweke nadhifu ukiwa na yeye nukia vizuri, harufu mbaya inamkirihisha ila*

*hawezi kukwambia.*
*
Usiwe na urafiki na waume walio na mtazamo mbaya kuhusu ndoa.*

*Watakuharibu mawazo.*
*
Mkeo ana thamani kubwa sana ndio maaana ukatoa vitu vya thamani*

*kumuoa, penzi lenu lifanye jipya, uzembe haufai.*
*
Kuzaa ni majaaliwa,* *mpende mkeo awe na watoto au asiwe nao,*

*usiwabague watoto kwa jinsia wafunze dini na watakuwa wacha*
*Mungu hadi maishani mwao.*
*
Hauwi mzee kwa mkeo katika kumburudisha, usiwe na ugomvi naye*

*mutakuwa katika kheri, usiwache kuwajali watoto wako na mkeo kwa*
*sababu ya wanawake wengine au sababu yoyote ile, wao ni wewe na*
*wewe ni wao.*
*
Mume anayedumu na ibada ana usalama, omba kila siku, muombee*

*mkeo na watoto.*
*
TUKIYAFANYA HAYA TUTAKUWA* *NA NDOA BORA MNO!!
*

