UPO SINGLE HUJUI TU


Upo SINGLE kwa sababu kila ukimtumia SMS hakujibu ,kila ukimpgia simu hapokei au hapokei kwa wakati. Anataka wewe ndo uwe una mpigia simu na kumtumia SMS,ukikaa kimya anauliza " Mbona upo Kimya sana?"
Hapo anajifanya kusahau idadi ya SMS zako ambazo unamtumia bila kujibiwa.
Upo SINGLE kwa sababu Mumeo au Mkeo anaweza rudi SAA 8 usiku au kesho asubuh huku kaz yake mwisho ni kila siku jioni. Hivyo hayo Massa alikuwa na mwenzako,ukimuuliza anakuwa mkali.
Hana biashara yoyote lakin anaweza toweka nyumban hata wik nzima usimuone na bila taarifa au kwa taarifa ya Uongo.
Upo SINGLE kwa sababu Umeolewa lakin kuanzia kula na kuvaa kwa watoto unahangaikia wewe,mwanaume wako kaz yake kuulizia tu chakula
Una mke lakin ndan ya nyumba kupika,kufua,kuwaangalia watoto ni juu yako. Mkeo hatak kupika anataka umuagizie chakula au mukale hotelin
Upo SINGLE kwa sababu mtu uliye nae hana wazozo lolote jipya la kuweza kukuinua au kuwainua kiuchumi. Kila unacho fanya ni juhud na mawazo yako.
Upo SINGLE kwa sababu mahusiano uliyo nayo huna furaha na unataman hata kesho yaishe,lakin unaendelea nayo ili kuwaaminisha watu kuwa una mpenzi.
Ifike mda fanya maamuzi,acha maisha ya kuigiza kupoteza mda na kuumiza akili yako juu ya mtu asiye jali uwepo wako katika maisha yake.
Kuwa katika mahusiano na mtu asiye kupa ushirikiano ni sawa upo SINGLE
May be an image of one or more people, footwear and indoor

DOWNLOAD APP YETU GOOGLE PLAY BONYEZA HAPA

DOWNLOAD APP YETU GOOGLE PLAY BONYEZA HAPA